Luke 10:25-28
25 aWakati huo mtaalamu mmoja wa sheria alisimama ili kumjaribu Isa, akamuuliza, “Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?” 26Isa akamjibu, “Imeandikwaje katika Torati? Kwani unasoma nini humo?” 27 bAkajibu, “ ‘Mpende Bwana Mwenyezi Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote’; tena, ‘Mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.’ ” 28 cIsa akamwambia, “Umejibu vyema. Fanya hivyo nawe utaishi.”
Copyright information for
SwhKC